News and Updates

NAFASI KIDATO CHA TANO 2024. USAJILI UMEANZA NA UNAENDELEA

Usajili kwaajili ya kujiunga na kidato cha Tano umeanza. HAKUNA INTERVIEW Mwanafunzi awe amepata Division 1 au II kwenye matokeo yake ya kidato cha nne.

Nini Chakufanya iliupate Nafasi?: Chukua fomu ya kujiunga, kisha ijaze kwa usahihi na irejeshe shuleni au kwanjia ya whatsapp no. 0753963866. Fomu ikishahakikiwa utapewa control no. kwaajili ya malipo ya ada. Itakupasa kulipia kiasi chochote (sehemu ya ada) kuanzi laki 3 ili kushika nafasi.

SHULE ZA GILI ZANUNUA KAMUSI KUU TOLEO JIPYA TOKA BARAZA LA KISWAHILI TANZANIA

Makabidhiano ya Kamusi Kuu toleo jipya baina ya Uongozi wa Baraza la Kiswahili  la Taifa na Uongozi wa Shule za Gili.Hakika idara ya lugha inaushukuru sana uongozi wa Gili kwa kukieshimisha sana Kiswahili kwani ujenzi wa Istilahi  bila Leksikografia ni ngumu. Kazi iendelee

ufadhili wa masomo kidato cha tano na sita

UFADHILI KIDATO CHA TANO NA SITA

Uongozi wa shule ya wasichana Gili High School unategeme kuwafadhili wasichana wachache katika masomo yao ya Kidato cha Tano na Sita. Ufadhili huo utagaramia garama zote za Ada na Michango mingine. 

Vigezo Vya kupata Ufadhili ni : Awe msichana aliyemaliza kidato cha nne 2023, Awe amefaulu kwa daraja la kwanza kwenye matokeo yake ya kidato cha nne.

Nini Ufanye: chukua fomu ya kujiunga jaza taarifa zako kisha irejeshe shuleni kabla au siku ya usaili. Usaili /Interview utafanyika tarehe 24/02/2024.